Friday, 14 August 2015

yanayoendlea mbeya muda huu





SONGWE INTERNATIONAL AIRPORT #MBEYA
UKAWA MEMBERS AND SUPPORTERS WAITING #HON_EDWARD_LOWASA










Saturday, 8 August 2015

LOWASSA AONGOZA KURA ZA URAIS.
Shirika la New Deal Africa kupitia mtandao wake wa Easypolls.com wanaendesha utafiti (opinion poll) kwa wagombea Urais nchini Tanzania waliojitokeza hadi sasa ambao ni Edward Lowassa wa (CHADEMA /UKAWA) na John Magufuli (CCM).
Hadi leo jioni matokeo ya mtandao huo yanaonesha kuwa uchaguzi ungefanyika leo Lowassa angeshinda kwa 64%, na Magufuli angefuatia kwa 31%, huku 5% ya wapiga kura wakiwa hawajaamua wampigie nani kati ya Lowassa na Magufuli.


Bila shaka hawa ni wale wanaosubiri wagombea wa vyama vingine wajitokeze. Kwa maana hiyo ni kwamba wagombea watakaojitokeza kupitia ACT, TADEA, CHAUSTA, na vyama vingine watagawana 05% ya hao "undecided".
Nawe pia unaweza kupiga kura yako na kumchagua Rais umtakaye kwa kubofya hapa host1.easypolls.net/poll.html?p=55c4c83de4b0e200525

ZITTO ADAI MAGUFULI SI MSAFI

Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli si msafi katika utendaji kazi wake kama inavyoelezwa kwa Watanzania.




Zitto alijenga hoja yake ya kumtuhumu Magufuli kuwa si msafi kwa kudai kuwa kuna Sh. bilioni 87/= “zimeibiwa” Wizara ya Ujenzi ambayo ndiyo anayoiongoza.
“Fedha hizi ni sehemu ya Sh. bilioni 252/= za miradi ya umeme, barabara na miradi maalumu zilizokosa maelezo yake kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali ambapo kukosekana kwa fedha hizo ni kiashiria cha kuwapo matumizi mabaya katika wizara iliyoongozwa na Magufuli,’ alisema Zitto.